CineBox
CineboxAugust 14, 2023BODI YA FILAMU YAFUNGUA DIRISHA LA KUPOKEA FILAMU KWA AJILI YA TAMASHA LA TUZO ZA FILAMU 2023   Akizungumza katika ufunguzi huo uliofanyika tarehe 11 Agosti, 2023 Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Dkt. Kiagho Kilonzo amesema lengo la uwepo wa Tamasha la Tuzo hizo ni kutambua mchango wa Wasanii na Wadau wote wa Filamu katika eneo hili la Filamu, kutambua vipaji vyao, kuwaongezea hamasa ya kuzalisha kazi nyingi zaidi za Filamu, kuwaongezea hamasa ya kuandaa kazi zenye ubora zaidi ili wawe na ushindani mkubwa ndani na nje ya Nchi, na kusisimua fursa za uwekezaji katika eneo hilo la Filamu nchini. Zoezi la upokeaji Filamu zitakazo shiriki katika Tamasha la Tuzo za Filamu Tanzania 2023 limeanza rasmi tarehe 11 Agosti 2023 na litadumu kwa wiki 6 hadi tarehe 25 Septemba 2023 ambapo Filamu zitapokelewa kwa njia Tatu ikiwemo, kuwasilishwa Ofisi za Bodi, Kwa njia ya Mtandao – https://taffa.info (mfumo utafunguka tar 17 Aug), pamoja na kuzifuata (Filamu) Mikoani katika mikoa 26 Tanzania Bara. Filamu zitakazo pokelewa zitahakikiwa na Majaji na zitakazopita katika Mchujo wa kwanza zitapata nafasi ya kuoneshwa kwa hadhira ili kupigiwa kura kupitia kituo cha Azam TV Chaneli ya Sinema Zetu (103), pamoja na vituo vingine vitakavyopenda kuonesha kazi hizo. Kura zitapigwa kwa njia mbili: njia ya ujumbe mfupi wa maneno (SMS), na kupitia mfumo wa kidijiti (https://taffa.info). Aidha, maelekezo mengine ya namna ya kupiga kura yataendelea kutolewa baada ya Mchujo wa kwanza kupitia mitandano ya kijamii ya Bodi ya Filamu. Pamoja na mambo mengine, Tamasha la Tuzo za Filamu Tanzania 2023 limeongeza wigo wa ushiriki wa Filamu kutoka Nchi za Afrika Mashariki ambazo zimeandaliwa kwa lugha ya Kiswahili ili kuendelea kuithamini na kuikuza lugha hiyo ambayo ni moja ya nembo ya Taifa letu. [...] Read more...
Admin CineboxAugust 12, 2023Kamati ya kuchagua Filamu ya Oscars Tanzania inatoa wito kwa watayarishaji wa filamu kuwasilisha filamu zao kwaajili ya Tuzo za 96 za Oscars. Vigezo vya kushiriki kwenye tuzo za Oscars. Ili filamu iweze kushiriki katika Tuzo za Oscars kwenye kipengele cha Filamu Bora ya Kimataifa (International Features Film), inatakiwa iwe na vigezo vifuatavyo. Filamu iwe imetayarishwa nje ya Marekani; Filamu iliyooneshwa kwenye nchi husika kwa kipindi cha kuanzia tarehe 1 Disemba, 2022 had 31 Oktoba, 2023 na ionyeshwe kwa angalau siku saba mfululizo katika kumbi za sinema za kibiashara kwa faida ya mtayarishaji na muoneshaji. Filamu iwe imetangazwa (Promotion)/ imeonyeshwa katika kumbi za Sinema; Filamu iwe na urefu kuanzia dakika 40; Filamu iwe imetumia lugha nyingine mbali na kiingereza kwa Zaidi ya 50%, ikiwa na Subtitles za kiingereza; Filamu iwe katika muundo wa Digital Cinema Package (DCP) kwa ubora wa angalau 2040 kwa 1080 pixels (2K); Filamu iwe na sauti ya kipimo cha 5.1 au 7.1, au iwe nyenye chaneli 3 za Sauti (left, right & centre). Angalizo: Filamu ambazo zilisambazwa au kufanyiwa maonyesho nje ya kumbi za Sinema hazikidhi vigezo kwenye Tuzo hizi. Maonesho hayo kwa umma ni: Filamu kuonyeshwa kwenye Cable Telesheni; Filamu isiwe katika PPV (Pay-Per-View) Video in Demand; Filamu isiwe kwenye usambazaji wa DVD; na Filamu isiwe imeonyeshwa/ imesambazwa kwenye ndege. Kusambaza kwenye mtandao wa Internet. Waandaaji waFilamu nchini wanaalikwa kuwasilisha filamu zinazokidhi vigezo vya ushiriki wa Tuzo hizi za Oscars ili ipatikane filamu moja itakayowasilishwa kwa waendeshaji wa Tuzo hizo nchini Marekani. Tarehe za kupokea Filamu Kamati itaanza kupokea filamu kuanzia tarehe 10 Agosti, 2023 hadi Tarehe 15 Septemba, 2023. Link za filamu zitawasilishwa kupitia: tanzaniaoscars@gmail.com. Kwa taarifa Zaidi, tembelea: Tanzania_oscars @instagram, @twitter, @facebook NB: Kwa Maoni au Maswali Tafadhali tuma Baruapepe kwenda: tanzaniaoscars@gmail.com   imetolewa na Dkt Mona Mwakalinga Mwenyekit wa Kamati 10/08/2023 [...] Read more...
CineboxJuly 24, 2023Dili za Mchongo ni filamu inayohusu uhasama kati ya magenge matatu ya mtaani yaani Genge la Mazombi ambalo linaongozwa na Biggie husika inayochezwa na Norriega Francis, Genge la wasogeza unga wasio na huruma la Chatara likiongozwa na wanzuki husika inayochezwa na Dark Master, Pamoja na genge la Nyati ambalo nalo linasogeza unga. Play boi Sizwe, muuza nyama anayependa mapenzi anajikuta katikati ya twimbili hili la magenge yasiyo na huruma. Filamu ya Dili za Mchongo imetayarishwa na Bongohoodz Pichaz ikiwa imeongozwa na Novatus Mugurusi ilitoka December 2022, kama trademark yao wammeendelea kutumia wasanii wakongwe wa bongo flava ambao wameigiza kwa ustadi mkubwa. Dili za mchongo inakuonyesha jinsi magenge ya mtaani yanavyofanya kazi na Maisha yao ya kila siku yapo vipi. Dili ya Mchongo ni moja ya filamu za bongo movie ambayo imepiga hatua kubwa kabisa katika kujaribu kukuonyesha life style ya wahuni wanaoishi kwenye magenge nakuona jinsi ambavyo hawana huruma katika makoso ikiwemo usnichi. Kwenye Dili za mchongo utafurahia sana kuona mapenzi ya wahuni yanavyoendeshwa, inaitaji ustaadi mkubwa kuweza kujenga mapenzi katika ya genge la wahuni, kama unavyoambiwa wahuni sio watu wazuri. Nguvu ya genge kuweza kufanya kazi ni hofu, basi ukizma kwenye filamu hii ya Dili ya Mchongo utaona jinsi ambavyo hofu inatumika vizuri katika kufanya mambo yatokee. Genge bila hofu hakuna Genge. Inaweza kuwa hofu ya umauti au hofu ya kukaa kitaa kukufakisha bila msaada wa mtu yeyote. Kwahiyo Hofu imetumiwa vizuri kwenye hii filamu. Mapenzi yana run dunia, Mapenzi yana run dunia ooooh!! Mapenzi ndio yanafanya dunia itembee, ila ukiwa kwenye magenge au mhuni basi unahitaji ustaadi mkubwa katika kujenga penzi. Kwenye pesa usnitch upo, kwenye pesa nyingi zaidi usnitch ni mkali zaidi, kwenye biashara ya dawa ya kulevya usnitch ni mkubwa zaidi, filamu nzima ya Dili ya Mchongo ni kuhusu snitch mmoja aliyendani ya genge la wasogeza unga, Ukizama katika Dili za Mchongo itakupeleka katika dunia ambayo huijui na utajionea jinsi gani kitaa kinaweza fakisha mtu yeyote, sio poa mzee. Usikose kutazama hii another one kutoka kwa Rrhac.  [...] Read more...